Home Habari za michezo KUELEKEA MECHI YA KESHO….YANGA WABET KWA BEKI WAO KUPATA USHINDI…NABI AANIKA KILA...

KUELEKEA MECHI YA KESHO….YANGA WABET KWA BEKI WAO KUPATA USHINDI…NABI AANIKA KILA KITU…

Habari za Yanga SC

Kocha Mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi, amefichua kuwa, uwepo wa beki mpya wa timu hiyo, Mamadou Doumbia raia wa Mali, utawasaidia kwa kiasi kikubwa kupata ushindi katika mchezo ujao wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Real Bamako.

Nabi ametoa kauli hiyo kuelekea katika mchezo huo wa Kundi D unaotarajiwa kupigwa Februari 26, mwaka huu nchini Mali, ikiwa ni baada ya kuwachapa TP Mazembe mabao 3-1, juzi Jumapili.

Yanga kabla ya kuelekea Mali kucheza na Real Bamako, juzi Jumatano ilipambana na KMC katika mchezo wa Ligi Kuu Bara na kuibuka na ushindi wa goli 1-0.

Nabi alisema kuwa, licha ya uwepo wa kipa Djigui Diara raia wa Mali ndani ya kikosi chake, lakini anaamini Doumbia atawasaidia kwa kiasi kikubwa kupata matokeo mazuri katika mchezo huo ili kufikia malengo ya kucheza robo fainali ya michuano hiyo.

“Tumemaliza kazi ya hapa nyumbani, lakini bado tuna kibarua kizito cha kuhakikisha timu inapata matokeo mazuri katika mchezo ujao, tutawatumia wachezaji wetu kutoka Mali, Doumbia na Diara ili kupata matokeo mazuri.

“Wapinzani wetu siyo timu ya kubezwa kwa sababu tumewafuatilia na tutaendelea kufuatilia mechi zao ili kupata namna bora ya kupata ushindi wa ugenini kwa sababu ukiangalia hawa tulionao watatusaidia sehemu kubwa kupata ushindi kule Mali ,” alisema Nabi.

SOMA NA HII  RASMI....YANGA WAKUBALI YAISHE KWA FEI TOTO KUJIUNGA SIMBA....WATOA MASHARTI HAYA MAGUMU KWA MO DEWJI....