Home Habari za michezo MORRISON AIBUKA UPYA YANGA…ALLY KAMWE ATOA KAULI YA KLABU…NKANE NAYE NDANI…

MORRISON AIBUKA UPYA YANGA…ALLY KAMWE ATOA KAULI YA KLABU…NKANE NAYE NDANI…

Habari za Yanga

Ripoti kutoka kwenye kambi ya Yanga zinasema kuwa kiungo wa pembeni wa klabu hiyo, Bernard Morrison ameshapona kwa asilimia 80 na muda siyo mrefu atarudi kwenye mechi za ligi na kimataifa.

Ripoti hiyo ilitolewa na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga, Ally Kamwe, ambaye alisema mambo ni mazuri kwa Morrison na wachezaji kama Denis Nkane ambao walikuwa majeruhi na tayari wameshaanza mazoezi.

“Timu ya wachezaji ambao wamebaki kwenye timu kwa kutoitwa kwenye timu zao za taifa wanaendelea vizuri na mazoezi na wale waliokuwa majeruhi wapo sawa.

“Nkane yeye ameshapona na yupo tayari kucheza mechi ya ushindani na kwa Morrison yeye amepona kwa asilimia 80, nafikiri kwenye mechi zijazo za ligi anaweza kuwa sehemu ya timu,” alisema.

Yanga wanajiandaa na mchezo wao wa mwisho wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya TP Mazembe utakaochezwa DR Congo. Baada ya hapo watarudi kujiandaa na Dabi ya Kariakoo dhidi ya Simba na Morrison anaweza akawepo kwenye mechi hiyo.

SOMA NA HII  KWA TAKWIMU HIZI....SIO AJABU KWA PACOME ALIVYOOMBWA JEZI NA MCHEZAJI WA CR BELOUIZDAD..