Home Michezo US MONASTR:- TUNAADHIMISHA MIAKA 100…MECHI NA YANGA USHINDI LAZIMA

US MONASTR:- TUNAADHIMISHA MIAKA 100…MECHI NA YANGA USHINDI LAZIMA

US MONASTR:- TUNAADHIMISHA MIAKA 100...MECHI NA YANGA USHINDI LAZIMA

Klabu ya Us Monastr ya Tunisia imefikisha miaka 100 tangu kuanzishwa kwake na kuelekea mchezo wa leo Jumapili Machi 19 wa kombe la shirikisho dhidi ya Yanga mwalimu Darko Novic ameahidi mchezo mzuri na ushindi kama sehemu ya kuadhimisha Sherehe za kutimiza miaka 100.

Yanga watakuwa na kibarua kizito cha kulipa kisasi mbele ya US Monastir na kuhakikisha pia wanajikatia tiketi ya kucheza Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Yanga wanahitaji alama tatu katika mchezo wa leo ili kujipatia tiketi wakati US Monastir wao wameshafuzu kwa hatua ya Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho.

Msimamo wa kundi D ulivyo mpaka sasa:
US Monastir: Michezo 4 alama 10
Yanga Michezo 4 alama 7
TP Mazembe: Michezo 4 alama 3
Real Bamako: Michezo 4 alama 1

SOMA NA HII  KIUNGO MGANDA AWACHANA MUDAHTIR NA BANGALA...AWATOBOLEA SIRI MECHI NA MAZAMBE

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here