Home Michezo WANAOKUSHANGILIA WATAKUJA KUKUCHEKA…KIUNGO SIMBA AMSHAURI FEISAL SALUM “FEI TOTO”

WANAOKUSHANGILIA WATAKUJA KUKUCHEKA…KIUNGO SIMBA AMSHAURI FEISAL SALUM “FEI TOTO”

Habari za Yanga

Akiwa na Takriban miezi minne pasipo kucheza mpira kutokana na mgogoro wa Kimkataba biana yake na Klabu yake ya Yanga huku taarifa za uhakika zikidai ni kudai maslahi.

Mchezaji wa Yanga, Kiungo Feisal Salum “fei toto” amepewa mbinu namna ya kupata maslahi anayoyadai kupitia kipaji chake.

Kiungo wa Simba anaeikipiga kwa Mkopo Ihefu, Mnigeria Victor Akpan, amemshauri Feisal namna ya kulipwa pesa ndefu kwa wachezaji wa kigeni.
Akizungumza Akpan amesema;

“Kuhusu Fei Toto, Mimi kama mchezaji ninayejua mchezo wa mpira ni wa muda mfupi naelewa anachopitia, wanaomshangilia leo akiwa staa watamcheka akistaafu kama hajajiwekeza kimaisha.

“Huenda kweli kakosea kuvunja mkataba, lakini Yanga wanaionaje thamani ya Fei Toto maana kwa sasa yupo kwenye kiwango cha juu asipopewa anachokitaka atapewa nyakati zipi, soka lina mambo mengi sana.”

SOMA NA HII  ULE MGOLI WA INONGA UMEANDIKA REKODI HII...UMEVUNJA REKODI YA OKWI

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here