Home Habari za michezo AL AHLY WAIKATAA YANGA MCHANA KWEUPEEEEE

AL AHLY WAIKATAA YANGA MCHANA KWEUPEEEEE

Mchezaji wa Al Ahly, Ali Maâloul amesema kuwa hawakuwa wanaijua Yanga SC, lakini walivyoingia hatua ya Makundi ndiyo wakaanza kuifuatilia.

Nyota huyo raia wa Tunisia amesema licha ya kutowafahamu vyema Yanga SC, lakini wamekuja Tanzania kwa ajili ya alama tatu.

Ahly wameshatua nchini tayari kwa ajili ya kuvaana na Yanga kesho Jumamosi kwenye mchezo wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika utakaopigwa katika Dimba la Mkapa.

Tangu mchezo wa kwanza dhidi ya CR Belouizdad tulianza kuifuatilia pamoja na majeruhi wote tuliowapata kwenye timu yetu, lakini bado tunaimani ya kuondoka na alama tatu hapa ugenini,” amesema Ali.

SOMA NA HII  YANGA YASAJILI MASHINE 4 KWA MPIGO,LUIS AKOMBA MIHELA, NDANI YA CHAMPIONI JUMATATU