Uncategorized

GADIEL MICHAEL AWAANGUKIA VIONGOZI NA MASHABIKI WA YANGA

admin July 10, 2019 11:28 am


GADIEL Michael, bieki mpya wa Simba ambaye amesaini kandarasi ya miaka miwili akitokea Yanga amewaomba radhi viongozi wa Yanga na mashabiki wake.

Kupitia ukurasa wa Instagram, Michael ameandika namna hii:-
“Wakati mwingine mtu unalazimika kufanya maamuzi yako peke yako kwa sababu anaewajibika na maisha yako mwisho wa siku ni mtu mwenyewe.

 “Mpira ndio kazi yangu ya kimaisha, maamuzi niliyoyafanya yalikuwa ni muhimu sasa kwa maslahi yangu na familia yangu.

“Nimuombe radhi aliyekuwa meneja wangu Jemedari Saidi Kazumari kutokana na sintofahamu iliyotokea kwa kutomshirikisha nikiamini asingekubali nihame mtaa.

 “Nimelazimika kufanya maamuzi magumu kwa maslahi mapana yangu mwenyewe na familia yangu.

 “Kikubwa ni kwamba Mpira ni familia moja, bado tuko kwenye familia,hakuna chuki maisha yaendelee.

“Niwashukuru wanaYanga wote kwa ushirikiano walionipatia, nilikuwa na furaha sana kwao. Pia niwashukuru viongozi wa Yanga chini ya mzee Msolla. Mimi ni mwanadamu, kiumbe dhaifu, Maana aliekamilika ni Mola wetu pekee. Nawaomba radhi sana,” amemaliza Michael.

BOVU LA MANARA KWA WACHAMBUZI KUHUSIANA NA SIMBA KUSAJILI “WAHENGA” TIMU YA TAIFA YA WANAWAKE TANZANITE KUSHIRIKI MICHUANO YA COSAFA, VIJANA WAPATA SHAVU

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply