Uncategorized

MBELGIJI WA YANGA KUTESTI MITAMBO LEO MBELE YA KAGERA SUGAR, TAMBO ZATAWALA

admin January 15, 2020 7:27 am

KOCHA Mkuu wa Yanga, Luc Eymael na msaidizi wake Riedoh Berdien ambao wamepewa kandarasi ya mkataba wa mwaka mmoja na nusu leo watakuwa na mtihani wao wa kwanza kutesti mitambo yao mbele ya Kagera Sugar, Uwanja wa Uhuru.
Kagera Sugar iliyo chini ya mzawa, Mecky Maxime mwaka 2020 ipo nafasi ya nane na imjikusanyia pointi 24 itakutana na Yanga iliyo nafasi ya saba na imejikusanyia pointi 25.
Yanga iliyokuwa chini ya Charlse Mkwasa imecheza mechi moja tu mwaka huu 2020 ilikuwa mbele ya Simba na ililazimisha sare ya kufungana mabao 2-2 uwanja wa Taifa, huku Kagera Sugar ikiwa imecheza jumla mechi mbili na imepoteza pointi sita ilifungwa bao 1-0 na Coatal Union pia ilifungwa mabao 2-1 na Polisi Tanzania.
Luc amesema kuwa mpango wake mkubwa ni kuona timu inapata matokeo mazuri kwenye mechi zake zote atakazocheza ikiwa ni pamoja nah ii ya leo dhidi ya Kagera Sugar huku kwa upande wa Maxime amesema kuwa anawatambua Yanga lazima apambane kupata pointi tatu muhimu.

TOTTENHAM WABISHI KWELI, WAIGOMEA MKWANJA WA INTER MILAN NA KUWAPA MASHARTI MENGINE AZAM FC KAZINI TENA EO MBELE YA LIPULI, TAIFA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply