Uncategorized

YANGA YATAJA ILIVYOWABANA SIMBA TAIFA, MASHABIKI WAPEWA TANO

admin March 10, 2020 6:57 am


NAHODHA Msaidizi wa Yanga, Juma Abdul amesema kuwa ilikuwa ni mpango kazi wa wachezaji kucheza kwa kujituma mwanzo mwisho kupata matokeo chanya kwenye mchezo wao wa watani wa jadi dhidi ya Simba na kuwashukuru mashabiki kwa kujitokeza kwa wingi.

Simba ilikubali kuchapwa bao 1-0 na Yanga kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa Uwanja wa Taifa, Machi 8 na kuziacha pointi tatu kusepa jumlajumla.

Akizungumza na Saleh Jembe, Abdul amesema kuwa wachezaji walipewa majukumu na kila mmoja alitimiza kile ambacho aliambiwa akifanye kwa wakati ndani ya uwanja.

“Wachezaji tulijituma uwanjani na tulikubaliana kufanya kazi kwa kushirikiana jambo ambalo lilitupa kujiamini na kufanya vizuri kwenye mchezo wetu ambao ulikuwa ni mgumu, shukrani kwa mashabiki kujitokeza wa wingi,” amesema. 

CORONA YASIMAMISHA LIGI KUU YA ITALIA KWA MUDA SIMBA KWENYE KIBARUA KINGINE KESHO MBELE YA SINGIDA UNITED

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply