Uncategorized

GSM NA YANGA SASA WAJA NA STAILI MPYA YA USAJILI

admin April 11, 2020 6:06 am
WADHAMINI wa Yanga, Kampuni ya GSM wamerejea kivingine klabuni hapo na safari hii wamekuja na staili mpya ya usajili kwa wachezaji wa kimataifa ambayo ili usajiliwe ni lazima uichezee timu ya taifa ya nchi yako.
Hiyo ikiwa ni siku chache tangu GSM watangaze kurejea kuendelee na udhamini wa nje ya mkataba ikiwemo posho, mishahara wa wachezaji na benchi la ufundi, kambi za wachezaji na usajili ambayo ilifanikisha usajili wa Bernard Morrison, Haruna Niyonzima, Ditram Nchimbi, Yikpe Gnaimen.
GSM imerejea Yanga ni baada ya hivi karibuni kutangaza kujiondoa kwenye udhamini wa timu hiyo kufuatia baadhi ya viongozi wa Kamati ya Utendaji kudai wadhamini hao wanaingilia majukumu ya viongozi likiwemo suala la usajili.
Mwenyekiti wa Yanga, Mshindo Msolla amesema kuwa kwa sasa wataendelea kufanya ushirikiano na GSM kwa kuwa ni wanafamilia na wanaipenda timu ya Yanga.

“GSM ni wanafamilia wa Yanga wanaipenda timu ndio maana wapo nasi bega kwa bega, wamekuwa nasi kwenye nyakati mbalimbali na wamefanya makubwa ikiwa ni pamoja na kutupa sapoti wakati wa kambi pale Tanga tulipocheza na Coastal Union hivyo bado kuna tupo nao pamoja,” amesema.
MUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA CHAMPIONI JUMAMOSI KIONGOZI SIMBA ALIPATA TABU SANA NA BAO LA MORRISON ALILITAZAMA KWENYE WHATSAPP

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply