Uncategorized

POLISI TANZANIA YAZIPIGIA HESABU POINTI TATU ZA LIPULI

admin June 20, 2020 10:47 am


SIXTUS Sabilo, mtupiaji namba moja ndani ya Klabu ya Polisi Tanzania amesema kuwa kazi kubwa waliyonayo ni kuendelea pale walipoishia wakati Ligi Kuu Bara iliposimamishwa kutokana na janga la Virusi vya Corona.

Hakukuwa na mechi ya ushindani tangu Machi 17 baada ya Serikali kusimamisha masuala ya michezo mpaka pale yaliporuhusisiwa kuanza kutimua vumbi Juni Mosi, na Juni 13 ligi ilianza ambapo leo Polisi Tanzania iliyo chini ya Kocha Mkuu, Malale Hamsini itamenyana na Lipuli ya Iringa.

Akzungumza na Saleh Jembe, Sabilo amesema kuwa kila mchezaji ana morali kubwa ya kusaka ushindi ili kupata pointi tatu.

“Kwenye mchezo kwetu muhimu pointi tatu, tuna amini kwa namna ambavyo tumejipanga kila kitu kitwenda sawa na tutapata pointi tatu ukizingatia kwamba tunacheza nyumbani mashabiki wajitokeze kwa wingi,” amesema.

Sabilo ametupia mabao saba ndani ya Polisi Tanzania iliyofunga mabao 29.

LIPULI IPO FITI KUWAVAA POLISI TANZANIA LEO NANGWANDA SIJAONA LEO KUNA BIASHA MOJA TU PEVU KWA WANAUME 22 KUSAKA POINTI TATU

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply