Uncategorized

SIMBA:TUNATAKA KUFIKA HATUA YA NUSU FAINALI LIGI YA MABINGWA

admin November 24, 2020 12:47 pm


UONGOZI wa Simba umeweka wazi kuwa kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika kwa msimu wa 2020/21 malengo yao makubwa ni kufika hatua ya nusu fainali.


Simba itacheza mchezo wa awali na Plateau United ya Nigeria kati ya Novemba 27-29 nhini Nigeria ambapo kikosi cha wachezaji 24 kinatarajia kuanza safari leo kwa kupitia Ethiopia.

Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara amesema kuwa mipango ipo sawa na wanaamini kwamba watakwenda kupambana ili kufikia malengo ambayo wamejiwekea kwa msimu wa 2020/21 ikiwa ni kuhakikisha wanapeperusha bendera ya Tanzania kimataifa.

“Mipango ipo sawa na kila mchezaji yupo tayari, tunakwenda kucheza soka safi na linaloeleweka ndani ya uwanja bila kufanya makosa kama msimu uliopita, mashabiki watupe sapoti,” amesema.
NYOTA MZAWA ANAYEWINDWA NA YANGA ATOA YA MOYONI SAKATA LA MKWANJA KUMPONZA RAIS WA CAF LAWAIBUA TFF

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply