Uncategorized

KIUNGO WA YANGA KUIBUKIA AFRIKA KUSINI

admin December 3, 2020 3:47 am

 


NYOTA wa kikosi cha Yanga kiungo Mapinduzi Balama muda wowote kuanzia sasa anaweza kupelekwa nchini Afrika Kusini kwa ajili ya kupatiwa matibabu zaidi.


Balama alipata maumivu ya mguu wa kushoto msimu uliopita wakati timu yake ikiwa kwenye maandalizi ya mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Ndanda FC.


Kwa sasa ameendelea kupewa huduma ya matibabu huku akishuhudia wenzake wakiendelea kupambana kupata matokeo ndani ya uwanja.


Daktari wa Yanga, Shecky Mngazija amesema kuwa kiungo huyo atakwenda Afrika Kusini ili kufanyiwa uchunguzi zaidi baada ya kukosekana uwanjani kwa muda mrefu.


“Ni kweli Balama Mapinduzi anaelekea Afrika Kusini kwa ajili ya kufanyiwa zaidi vipimo vya afya yake ili kuendelea mchakato na maendeleo yake.


“Taarifa zake tutaendelea kuzitoa kwani kwa sasa bado hatujajua kwamba itamchukua muda gani huko,” amesema.


Mapinduzi atakumbukwa kwa uwezo wake wa mashuti akiwa nje ya 18 ambapo aliibuka shujaa kwenye dabi dhidi ya Simba alipomtungua Aishi Manula na kufanya Simba isiamini ilichokiona kwani baada ya dakika 90 ngoma ilikuwa 2-2.

MUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA SPOTI XTRA ALHAMISI MRITHI WA FRAGA NDANI YA SIMBA KUANZA KUONYESHA MAKEKE YAKE, WENGINE WANAKUJA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply