Tetesi za usajili Yanga
Habari za michezo

YAO NA SOMO KWA WAZAWA MAMBO YAPO HIVI

Staff Desk October 7, 2023 12:55 pm

Ujio wa Diarra ulikuja kutuonyesha Utofauti na Ubora wa makipa wetu tuliokuwa tunaamini ni bora kwa muda mrefu,

Pia hata kwa Yao amekuja kutuonyesha maana halisi ya Mlinzi bora wa pembeni anatakiwa afanye awapo Uwanjani,

NANI KASEMA KIBWANA SHOMARI AMESHUKA KIWANGO ?

Yawezekana ndilo neno linaloongoza kukaa midomoni mwa watu pindi wasipomuona kiwanjani ama akiwa kwenye mbao ndefu,

Jua kwamba Usajili wa Yao ndani ya Yanga ulikuwa na lengo la kupata mlinzi mzoefu na mwenye Ubora katika eneo la upande wa kulia wa Young Africans katika Michezo ya kimataifa,

Ubora wa Yao kouassi umetengeneza tabaka kubwa sana Kibwana Shomari, hapa nazungumzia Ubora wake awapo Uwanja katika maeneo 3 kwa maana kujilinda, kuchezesha na kushambulia,

Yao Kouassi hajaleta utofauti na kibwana Shomari tu bali ameleta tupate darasa kwa walinzi wote wa pembeni zaidi ni wale wanaocheza Upande wa upande wa kulia,

Kwasasa ndani ya NBC ni vigumu sana kumlinganisha Mlinzi Yao na walinzi wengine, na hii ni kutokana Ubora wake mkubwa,

Yao ameleta Utofauti mkubwa sana na Tuliokuwa tuna amini ni bora kwa Upande wa kulia na ndio maana tumekuwa tukiona On and Off zao kwasasa kupitia Ubora na matukio ya Yao awapo Uwanjani,

Sio kwamba Yao bora sana ila ametuonyesha Ubora wake kwa zaidi ya 70% katika eneo analokuwepo yaani

Kujilinda

Kuchezesha/kutengeneza

Kushambulia

Utofauti na Wazawa Wamekuwa wakikupa kimoja kati ya 3 kwa Ubora iwe kujilinda ama kushambulia,

Yao ndio darasa halisi la mlinzi bora wa kulia anavyotakiwa kucheza na matukio yote Uwanjani.

HAYA SASA SIMBA YAPEWA WYDAD…… YANGA KUMALIZANA AL AHLY UGENINI SIMBA NI NGUMU ILA INAFUNGIKA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply