- Habari za michezo
- Habari za Yanga
- Habari za Yanga Leo
- Michezo
- Michezo Bongo
- Michezo Soka la Bongo
- news
- Simba SC
YAKUFANYA HAYA HAPA
HESHIMA
Katika orodha ya klabu bora za Afrika, Simba ipo juu ya Berkane ikishika nafasi ya nne wakati timu hiyo ya Morocco iko katika nafasi ya tisa, huku vinara wakiwa ni Al Ahly ya Misri, Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini, Esperance ya Tunisia zilizopo katika Tatu Bora.
Ukiachana na heshima ya kubeba kombe hilo, Simba ina kila sababu ya kukomaa kesho ili kukomba mabilioni ya fedha zinazotolewa kwa bingwa wa Kombe la Shirikisho Afrika.
Simba iliyoasisiwa mwaka 1936 ilianza michuano ya msimu huu katika raundi ya pili ikivaana na Al Ahli Tripoli ya Libya iliyoifunga kwa jumla ya mabao 3-1, ikitoka suluhu ugenini mjini Tripoli kisha kushinda 3-1 nyumbani na kutinga makundi ambapo iliwekwa katika Kundi A.