
Takwimu za mwaka 2024/25 kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) zinaonesha kuwa kwa sasa Tanzania hutumia zaidi ya lita milioni 60 za mafuta kwa mwaka, jambo linaloashiria ukuaji wa haraka wa sekta ya usafiri na ongezeko la mahitaji ya vilainishi bora.