Uncategorized

EMMANUEL OKWI AIVURUGA SIMBA

admin June 29, 2019 1:03 pm

NYOTA wa timu ya Simba, Emmanuel Okwi ambaye kwa sasa anazidi kuwa mtamu kwenye michuano ya Afcon inayoendelea nchini Misri amewavuruga mabosi wa Simba baada ya kutoweka wazi hatma yake ya kurejea Simba.

Okwi mpaka sasa kwenye michezo miwili ya Afcon ambayo Uganda wamecheza dhidi ya Congo pamoja na Zimbabwe amefunga mabao mawili na kuibuka mchezaji bora kwenye mchezo mmoja dhidi ya Congo hali inayomuongezea thamani.

Okwi amesema kuwa anajivunia kuwa na mashabiki wa Tanzania hali inayompa furaha hivyo wakati ukifika kila kitu kitakuwa sawa kwake kutaja hatma yake na Simba.

“Nafurahi kuwa na mashabiki wengi kutoka Tanzania nawapenda, kuhusu kurejea Simba kwa sasa ni ngumu kulizungumzia ila wakati ukifika itafahamika tu,” amesema Okwi.

Mtendaji Mkuu wa Simba Crescetius Magori amesema kuwa kwa sasa wanafanya mazungumzo na wachezaji waliomaliza mkataba endapo watafikia makubaliano watawasainisha ili kuendelea kupata huduma zao.

MWINYI ZAHERA WA YANGA AGOMA KUREJEA BONGO KINDA WA TIMU YA TAIFA YA ENGLAND APIGWA PINI MIAKA MITANO UNITED

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply