Uncategorized

KOCHA STARS:TUNAKWENDA KUPINDUA MEZA KIBABE KENYA

admin July 31, 2019 5:04 am

ETTIENE Ndayiragije Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ amesema kuwa sare waliyoipata sio mbaya wanakwenda kupindua meza nchini Kenya.

Stras ililazimisha sare ya bila kufungana na timu ya Taifa ya Kenya kwenye mchezo wa kwanza wa kutafuta tiketi ya kushiriki michuano ya Chan uliochezwa uwanja wa Taifa.

Ndayiragije amesema:”Perfomance yetu ilikuwa nzuri licha ya kushindwa kupata matokeo ila kikubwa ni kwamba wachezaji walikuwa bado hawajazoeana awali ni kazi kubwa ambayo kwa sasa tunaifanya.

“Hatujaruhusu bao ni kitu chanya hivyo hatuna presha  ya kulazimisha sare mchezo wa marudio, makosa ya kushindwa kumaliza nafasi tulizozitengeneza tayari tumeanza kuyafanyia kazi hivyo tunakwenda kutafuta matokeo chanya.

“Wachezaji wetu wameshaanza kuzoeana tofauti na mwanzo walikuwa bado wageni ila wamepambana kwa hali na mali,” amesema.

Mchezo wa marudio unatarajiwa kuchezwa Agosti 4 nchini Kenya na ili kufuzu michuano hii ni lazima Stars ishinde.

YANGA: KWA KIKOSI HIKI, MSIMU UJAO TUTAKUWA JUU ZAIDI MUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA CHAMPIONI JUMATANO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply