Uncategorized

JERRY MURO AIBUKIA TENA YANGA

admin August 18, 2019 12:51 pm


MKUU wa Wilaya ya Arumeru ambaye aliwahi kuwa ofisa habari wa Yanga Jerry Muro ameshangaa wanaodai timu yao ni dhaifu.

“Nani anasema Yanga mbovu, Yanga ni bora msimu huu kuliko timu yoyote wala isipimwe uwezo wake kwenye hizi mechi mbili tatu kwani itakuja kufanya balaa siku za usoni,” alisema Muro.

Straika mwenye nafasi kwenye kikosi cha kwanza, Juma Balinya nae akaongeza kwamba; “Mpira siku zote una matokeo tofauti, wakati mwingine unaweza ukapata matokeo chanya na muda mwingine unapata matokeo hasi kwahiyo mashabiki wanapaswa kuyakubali matokeo haya.”

“Wanachotakiwa kuamini ni kwamba mambo mazuri yanakuja hivyo wasiwe na wasiwasi,” alisema Balinya ambaye ni raia wa Uganda.

MBELGIJI SIMBA AWAGOMEA WABRAZIL VAR INAWALIZA KINOMA MANCHESTER CITY, GABRIEL JESUS HAAMINI KABISA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply