Uncategorized

MSEMAJI WA YANGA MPYA YANGA APATIKANA

admin August 30, 2019 1:32 pm


Tunaweza kusema kuwa kile kilio cha mashabiki na wanachama wengi wa Yanga kutaka Dismas Ten aondolewe katika nafasi ya usemaji na badala yake atafutwe mtu mwingine inaweza kuwa imepatikana.

Taarifa zinasema kuwa mwanachama na shabiki wa Yanga, Antonio Nugaz, ambaye pia ni mtangazaji katika kituo cha Clouds Media Group, anatajwa kuchukua nafasi ya Dismas Ten.


Nugaz ambaye amekuwa akijitahidi kuhudhuria mechi nyingi za Yanga, leo ameonekana akiwa na Dismas Ten ambaye alikuwa kwenye nafasi hiyo.

Taarifa zilizo ndani ya Yanga zinasema kuwa Nugaz anaweza akatangazwa muda wowote kuanzia sasa kurithi nafasi hiyo iliyopooza kama mashabiki wengi wa Yanga wanavyosema.


NAMBA 17 YANGA YALETA SINTOFAHAMU CR 7 ACHEKELEA USHINDANI WAKE NA MESSI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply