Uncategorized
EYMAEL WA YANGA AZIPIGIA HESABU POINTI TATU ZA RUVU SHOOTING NAMNA HII
LUC Eymael, Kocha Mkuu wa Yanga amesema kuwa leo vijana wake watapambana kuzipata pointi tatu za Ruvu Shooting.
Yanga inashuka Uwanja wa Uhuru kumenyana na Ruvu Shooting kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara majira ya saa 10:00 jioni.
Eymael amesema;” Mazoezi ambayo wameyafanya yanawapa nguvu ya kupambana, tunatambua kwamba utakuwa mchezo mgumu kwetu ila tutapambana kupata pointi tatu, mashabiki wajitokeze kwa wingi kutupa sapoti,”.
Mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Uhuru, Yanga ilipoteza kwa kufungwa bao 1-0 lililofungwa na Sadat Mohamed hivyo mchezo wa leo utakuwa ni wa kukata na shoka.
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.