Uncategorized

HIKI NDICHO KILICHOMCHELEWESHA MKUDE KUJIUNGA NA KAMBI YA TIMU YA TAIFA STARS

admin March 20, 2020 2:31 pm

JONAS Mkude, nyota wa Simba amesema kuwa sababu kubwa inayomfanya ashindwe kujiunga na timu ya Taifa ni matatizo ya kibinadamu yanayomkabili na siyo suala la utovu wa nidhamu.

Mkude alichelewa kujiunga na timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars iliyokuwa imeweka kambi kwa ajili ya kujiwinda na michuano ya CHAN iliyotarajiwa kufanyika nchini Cameroon hivi karibuni kabla haijaahirishwa kutokana kuzuia maambukizi ya Virusi vya Corona.

Mkude amesema: “Haina maana kwamba mimi ni mtovu wa nidhamu ndio maana ninachelewa kujiunga na timu ya Taifa hapana ninaithamini kazi yangu lakini masuala ya kibinadamu ndiyo ambayo yamekuwa yakinitatiza nishindwe kuwahi kwenye kambi,”.

Kocha Mkuu wa Stars, Ettiene Ndayiragije alisema kuwa hawezi kumzungumzia Mkude kwa kuwa hakuripoti kambini.

VIWANJA HIVI NI ADUI MKUBWA WA MAENDELEI YA SOKA TANZANIA BREAKING: MUUAJI WA SIMBA AREJESHA MKATABA YANGA, SASA UHAKIKA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply