Uncategorized

KAKOLANYA AAMBIWA ASEPE NDANI YA SIMBA KUPATA CHANGAMOTO MPYA

admin April 14, 2020 5:57 am


GOLIKIPA wa zamani wa timu ya taifa, Taifa Stars, Ivo Mapunda, amemshauri kipa wa Simba, Beno Kakolanya kwenda kutafuta changamoto nje ya nchi ili kulinda kipaji chake alichonacho cha kuokoa michomo golini. 

Kakolanya alijiunga na Simba kwenye msimu huu wa Ligi Kuu Bara akitokea Yanga baada ya mkataba wake wa miaka miwili ya kuichezea timu hiyo kumalizika. 

Kipa huyo tangu ametua kujiunga na Simba, amekuwa hapati nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo huku akimuachia Aishi Manula ambaye ndio pendekezo la kwanza la Mbelgiji, Sven Vandenbroeck. –

 Mapunda amesema kuwa Kakolanya ni kati ya makipa bora nchini ambaye anaamini kama akitoka kwenda kucheza nje ya nchi, thamani yake itaongezeka tofauti na ilivyo hivi sasa.

HOFU YA TAMBWE IPO KWA MEDDIE KAGERE VIFUAVIWILI:WATANIELEWA TU SIKU MOJA LICHA YA KUNIBEZA KWA SASA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply