Uncategorized

BOB HAISA AREJEA NA PENZI LA KARAHA

admin April 15, 2020 5:57 am


BOB Haisa, msanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye anaimba mtindo wa mduara amesema kuwa amerejea tena kwenye fani hiyo akiwa na kigongo kipya ambacho anaamini kitamrejesha kwenye chati.

Ngoma yake ya ‘Nipe Mgongo’ ilimpa mafanikio makubwa na kumfanya ajulikane nje na ndani ya nchi kwa sasa kigongo chake kipya kinaitwa Penzi la Karaha.

Akizungumza na Saleh Jembe, Bob Haisa amesema kuwa ni wimbo mzuri ambao una ujumbe kwa kila anayependa muziki mzuri.

“Kazi nzuri kwa watu wazuri na nimerejea kwa mtindo wa kipekee kwani uwezo wa kuimba na kuandika upo hivyo ni kazi kwa mashabiki kupata kile wanachokipenda,” amesema.


NIYONZIMA: AFYA NI MUHIMU, TUCHUKUE TAHADHARI NYOTA WA MTIBWA SUGAR AJICHIMBIA FUKWENI KUPIGA MATIZI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6131

Leave a Reply