Uncategorized

SHEVA: MUNGU AMETENDA MAAJABU NIPO KAMILI GADO

admin May 20, 2020 6:47 am


MIRAJ Athuman, ‘Sheva’ kiungo mshambuliaji ndani ya Klabu ya Simba amesema kuwa anamshukuru Mungu kwa kuwa ametenda maajabu kwa sasa yupo fiti.

Akizungumza na Saleh Jembe, Sheva amesema kuwa kwa sasa ameanza mazoezi binafsi pamoja na yale ya pamoja akiwa na wenzake jambo linalompa matumaini ya kuwa bora zaidi.

“Nipo vema ninamshukuru Mungu kwa kuwa tayari nimeanza mazoezi na wenzangu pamoja na yale binafsi jambo ambalo linanipa matumaini ya kuwa bora,” amesema.

Sheva ametumia dakika 508 uwanjani kwenye mechi za Ligi Kuu Bara amefunga mabao sita na kutoa pasi moja ya bao iliyokutana na guu la kulia la Meddie Kagere alikuwa nje kutokana na kusumbuliwa na jeraha la funda la mguu.

BAKARI MWAMNYETO ATAJA VIPAUMBELE VYAKE ILI ASAINI MCONGO HUYU MTUPIAJI ANASUBIRI SIMU YA YANGA ATUE MAZIMA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply