Uncategorized

WACHEZAJI WA CHELSEA KUWEKEWA MSOSI KWENYE GARI

admin June 4, 2020 4:47 pm


KLABU ya Chelsea imepanga kuwapelekea chakula wachezaji wake ndani ya gari baada ya mazoezi ili kujenga miili yao kutokana na sheria ya kuzuia mijumuiko isiyo ya lazima kuendelea.

Sheria hiyo ina lengo la kupunguza maambukizi ya Virusi vya Corona ambavyo vilisababisha kusimamishwa kwa shughuli nyingi duniani ikiwa ni pamoja na michezo.

Kwa sasa matumizi ya kanteen kwa wachezaji pamoja na wafanyakazi yamekatazwa jambo ambalo limewafanya viongozi kufikiria mbinu mbadala ya kuwapa chakula wachezaji wao wanaojiandaa na kurejea kwa Ligi Kuu England Juni 17.

Imeripotiwa kuwa wakati Kocha Mkuu, Frank Lampard akiwa anakinoa kikosi chake wapishi watakuwa jikoni wakipika na kuweka msosi ndani ya gari la kila mchezaji ambao ataufinya na mwingine kwenda nao nyumbani.

SERIKALI YAZUNGUMZIA KUHUSU SIMBA NA YANGA KUKUTANA FA YANGA YASTUKA DILI LA MAKAMBO, NDANI YA CHAMPIONI IJUMAA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply