Uncategorized

KIUNGO WA YANGA MORRISON AOMBA APANGWE KIKOSI CHA KWANZA AIMALIZE SIMBA

admin July 11, 2020 10:47 am

 BERNARD Morrison, kiungo mshambuliaji wa Yanga, amesema kuwa anamuomba Kocha Mkuu, Luc Eymael ampange kwenye mchezo huo ili afanya kazi yake mbele ya Simba.

Yanga itamenyana na Simba, kesho Julai 12 Uwanja wa Taifa majira ya saa 11:00 jioni kwenye mchezo wa hatua ya nusu fainali ya Kombe la Shirikisho.
Morrison alikuwa na mvutano wa kimkataba na masuala ya nidhamu na baadhi ya viongozi wa klabu yake ila kwa sasa amesharejea kambini na alikuwa kwenye kikosi kilichoshinda bao 1-0 mbele ya Kagera Sugar kwenye mchezo wa ligi.
Morrison amesema: “Nikipata nafasi ya kucheza nitaendelea kulinda heshima yangu na ya klabu, muhimu naomba Mungu niwe na afya njema kisha kocha anipe nafasi ya kucheza.

“Ninachohitaji ni sapoti ya mashabiki ambao wamekuwa wakiniunga mkono tangu nimefika hapa Tanzania, kama timu tunataka kuendelea pale tulipoishia.
  
 “Tunahitaji matokeo mazuri ili kupata nafasi ya kucheza michuano ya kimataifa msimu ujao, muhimu naomba kocha anipe nafasi kama nitakuwa fiti kiafya kisha mashabiki watuunge mkono katika mchezo huo muhimu.”
KUMUONA MORRISON AKIFANYA YAKE TAIFA MBELE YA SIMBA BUKU 10 TU MTUPIAJI NAMBA MOJA KWA WAZAWA AFUNGUKA ISHU YAKE NA KOCHA MKUU PAMOJA NA WACHEZAJI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply