Uncategorized

SIMBA QUEENS 5-0 BAOBAB QUEENS, YAIVUA UBINGWA JKT QUEENS

admin August 5, 2020 3:47 pm

TIMU ya Simba Queens leo Agosti 5 imeibuka na ushindi wa mabao 5 -0 mbele ya  Baobab Queens kwenye mchezo wa Ligi ya Wanawake uliochezwa Uwanja wa Uhuru.

Mabao ya Simba yalifungwa na Mwanahamisi Omary aliyetupia mawili,Opah Clement alitupia bao moja, sawa na Dotto Evarist  huku kipa Zubeda Mgunda akitupia bao moja kwa mkwaju wa penalti.

Ushindi wa leo unaifanya Simba Queens kutangazwa kuwa mabingwa wa Ligi ya Wanawake kwa kuwa wamefikisha jumla ya pointi 53 ambazo hazitaweza kufikiwa na timu yoyote kwa sasa ndani ya ligi hiyo.

Imebakiwa na mechi mbili za kucheza ambazo ni dhidi ya Alliance Girls  na TSC Queens yote hiyo itakuwa kanda ya ziwa Ushindi huo unaifanya kuivua JKT Queens ubingwa jumlajumla kwa kuwa msimu uliopita ilitwaa taji hilo.

NYOTA HAWA WATATU WA YANGA, MMOJA AMEACHWA MAZIMA,WAWILI MAMBO HAYAELEWEKI RUVU YAPIGA PANGA WATANO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply