Uncategorized

UNITED BADO HAWAJAMPOTEZEA SANCHO

admin September 28, 2020 3:47 pm

 


MANCHESTER United imesema kuwa itatumia nguvu kubwa kumpata nyota wa Borrusia Dortmund, Jadon Sancho ambaye inaelezwa kuwa yupo kwenye rada za mabosi hao.


Sarakasi za kuipata saini ya Sancho kuibukia Manchester United zimekuwa zikiripotiwa kukwama mara kwa mara ambapo United inaelezwa kuwa iligomea dau ambalo mabosi hao walitaja.


Dortmund inahitaji euro milioni 100 ili kumuachia nyota huyo kuibuka ndani ya Old Trafford.


Kocha Mkuu wa Manchester United, Ole Gunnar amesema kuwa kwa sasa ni ngumu kuweka wazi kuhusu masuala ya usajili ambapo mpango wa kusajili mabeki kwenye kichwa chake haupo.


“Bado kuna uhitaji sehemu kadhaa lakini kwa upande wa mabeki nina amini kwamba hawa waliopo watafanya vizuri,” amesema.

MBWANA SAMATTA AANZA NA SARE UTURUKI TFF YATOA ONYO KWA YANGA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply