Uncategorized

MENEJA WA KIUNGO WA PLATEU UNITED ANAYEWINDWA NA YANGA AFUNGUKIA DILI HILO

admin December 13, 2020 11:47 am


MENEJA wa nyota wa Plateau United, Isah Ndala amesema kuwa mchezaji huyo ana ofa nyingi kutoka timu mbalimbali ambazo zinahitaji kupata saini yake ikiwa ni pamoja na Yanga.

Ibrahim Ahmed ambaye ni meneja amesema kuwa mchezaji wake amekuwa akiwaniwa na timu nyingi kutokana na uwezo wake ndani ya uwanja.


Miongoni mwa timu ambazo zinatajwa kuwania saini yake ni pamoja na Yanga ambao walivutiwa na uwezo wake baada ya kucheza na Simba kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya awali.


Ahmed amesema:”Zipo timu nyingi ambazo zinaiwania saini ya mchezaji Ndala kwa sababu ana uwezo mkubwa na anajiamini hivyo nina amini kwamba ikiwa kuna timu itapata saini yake basi itapata faida kubwa.


“Kwa Tanzania zipo timu ambazo tumeanza mazungumzo nazo ikiwa ni pamoja na Yanga ila siwezi kusema kwamba kwa sasa tumefikia wapi na nini kiandelea kwa kuwa ni siri,” .


VANDENBROECK KUTUMIA JEMBE JINGINE LA KAZI KWA MBEYA CITY KIKOSI CHA SIMBA KITAKACHOANZA LEO DHIDI YA MBEYA CITY

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply