Uncategorized

MUANGOLA WA YANGA SAFARI YA KUSEPA IMEWADIA

admin December 22, 2020 4:47 am



CARLOS Carlinhos raia wa Angola mwenye uwezo wa kupiga mipira iliyokufa ndani ya kikosi cha Yanga huenda akatolewa kwa mkopo ama akaachwa Jumlajumla ndani ya kikosi hicho.

Habari zinaeleza kuwa kutokana na kusumbuliwa na majeraha ya mara kwa mara ni sababu ya nyota huyo kuwekwa kando kwa kuwa ameshaondolewa kwenye mfumo.

Muangola huyo anasumbuliwa na majeraha ya nyonga ambayo aliyapata alipokuwa mazoezini jambo.

Hakuwa kwenye kikosi kilichoshinda mabao 3-1 dhidi ya Dodoma Jiji na hatakuwa sehemu ya kikosi kitakachoivaa Ihefu kesho,Desemba 23 Uwanja wa Sokoine.

Hassan Bumbuli, Ofisa Habari wa Yanga kuhusu suala hilo amesema kuwa kwa sasa wanajiendesha kidijidatal hivyo kila kitu kitawekwa kwenye mitandao yao.

Yanga ikiwa imetupia jumla ya mabao 25 amehusika kwenye mabao manne, amefunga mawili na ana pasi mbili za mabao.

MUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA SPOTI XTRA JUMANNE ISHU YA MZAMBIA KUIBUKIA NDANI YA SIMBA IMEKAA NAMNA HII

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply