Uncategorized

TAULO LA JUMA KASEJA LAZUA ‘TIMBWILI’ MBEYA

admin January 3, 2021 6:47 am

 


 KIPA namba moja wa Klabu ya KMC, mkongwe Juma Kaseja aliingia kwenye mzozo na shabiki mmoja anayedhaniwa kuwa ni wa Klabu ya Mbeya City. 

Shabiki huyo aliibuka ndani ya Uwanja wa Sokoine dakika za lala salama baada ya kuona lango la KMC timu yake inakwama kufunga bao kwa kukosa nafasi nyingi jambo lililomfanya ahitaji kusepa na taulo la Kaseja lililokuwa langoni.

Baada ya Kaseja kuona taulo linasepa aliamua kuacha lango wazi huku mpira unaendelea na kufuata taulo lake na kulibakiza taulo lake langoni.


Kuhusu ishu hiyo Kaseja amesema:”Taulo halikuwa langu jambo lililonifanya nilifuate kwa yule ambaye alichukuwa kwa kuwa sikuwa na chaguo.


“Nilifanya hivyo kutokana na hali ya hewa ya Mbeya niliazima hotelini ili niwe nafuta gloves zangu zikilowana au mvua ikizidi niwe najifuta usoni hakuna kingine kwani ningemuachia ningedaiwa hotelini.”


Kwenye mchezo huo timu zote zilitoshana nguvu bila kufungana na kugawana pointi mojamoja.

SPURS WAENDELEZA MAKALI,KANE NA SON NI HABARI NYINGINE NYOTA YANGA AGOMBANIWA NA TIMU ZA LIGI KUU BARA ZIKITAKA SAINI YAKE

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply