Simba SC

WINGA MKONGO AFUNGUKIA DILI LAKE SIMBA

admin January 20, 2021 2:47 pm


BAADA ya kiungo Mkongo Karim Kinvuid Kiekie kuhusishwa kumalizana na klabu ya Simba, hatimaye kiungo huyo amefunguka kuwa hajafanya mazungumzo na uongozi wa Simba

Kiekie alicheza katika mchezo wa kirafiki kati ya Tanzania na Congo uliofanyika katika Uwanja wa Mkapa jijini Dar na kumalizika kwa sare ya bao 1-1,kwa sasa kiungo huyo yupo katika kiosi cha timu hiyo kinachoshiriki michuano ya CHAN inayoendelea kufanyika nchini Cameroon.

Akizungumzia kuhusu dili hilo Kiekie amesema: “Sijafanya mazungumzo na Simba juu wao kuhitaji huduma yangu, yote ambayo unayasikia wewe na mimi ninayasikia hivyohivyo ndio maana nayaacha yabaki kuwa tetesi ila kama itatokea wananihitaji basi kila kitu kitafahamika,”

Kiekie mwenye umri wa miaka 19 kwa sasa anakipiga katika klabu ya DC Motema Pembe ya nchini Kongo ambapo  nchini humo anachukuliwa kama mmoja kati ya wachezaji bora wanaochipukia kwa kasi.

MRUNDI WA YANGA AWAAHIDI MASHABIKI FURAHA CHIKWENDE ATAJA KITAKACHOMBEBA SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply