Simba SC

MAKIPA WAWILI WA SIMBA WAWEKA REKODI YAO CAF

admin March 23, 2021 11:47 am


 KIPA namba moja wa Klabu ya Simba, Aishi Manula ameweka rekodi ya kucheza jumla ya mechi tatu kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika bila kufungwa hatua ya makundi.

Wakati Manua ambaye ni kipa namba moja akiweka rekodi ya kukaa langoni bila kufungwa na kipa namba mbili naye Beno Kakolanya naye amekaa langoni mechi moja bila kupoteza.

Makipa wawili wa Simba wameweza kuweka rekodi kwenye hatua ya makundi kwa kucheza mechi nne bila kufungwa ambazo ni dakika 360 bila kuokota mpira wavuni.

Manula amekaa langoni kwenye mechi tatu ambazo ni dakika 270 ilikuwa AS Vita 0-1 Simba, Simba 1-0 Al Ahly 0 na Simba 3-0 Al Merrikh.

Kakolanya kipa namba mbili yeye kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambayo yanasimamiwa na Shirikisho la Soka Afrika, (Caf) amekaa kwenye mechi moja ilikuwa Al Merrikh 0-0 Simba.

KUMBE YANGA WALIWAPIGA BAO KAIZER CHIEFS KWA KISINDA NA MUKOKO TATU BORA ZA MAGUFULI MSIMU WA 2015/16 ILIKUSANYA MABAO 162

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply