Simba SC

SIMBA KAMILI KUIVAA POLISI TANZANIA

admin June 15, 2021 6:47 am


UONGOZI wa Simba umeweka wazi kwamba upo tayari kwa ajili ya mechi zao ambazo zimebaki ndani ya ligi ikiwa ni pamoja na ule dhidi ya Polisi Tanzania.

Mchezo wao ujao kwenye ligi unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Ushirika, Moshi baada ya ule wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Mkapa ubao kusoma Simba 2-0 Polisi Tanzania.

Akizungumza na Soka la bongo, Meneja wa Simba, Patrik Rweyemamu alisema kuwa maandalizi ya kikosi kwa mechi ambazo zimebaki yapo vizuri.

“Tupo vizuri kwa ajili ya mechi zetu ambazo zimebaki na mchezo wetu ujao pia tunaamini kwamba tutapambana ili kupata pointi tatu, mashabiki watupe sapoti kwani timu ilianza mazoezi Juni 8,” alisema Rweyemamu.

Kwenye msimamo wa ligi, Simba ipo nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 67 inakwenda kukutana na Polisi Tanzania iliyo nafasi ya 6 na pointi 41. 

ARGENTINA YATOSHANA NGUVU NA CHILE COPA AMERICA, MESSI ATUPIA KWA PIGO HURU VIDEO: WAZEE WA YANGA WAIKANA KATIBA MPYA, SIMBA YATUA KWA KIUNGO MNAIJERIA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply