kimataifa

GRIEZMANN AIBEBA UFARANSA IKIBANWA MBAVU EURO

admin June 20, 2021 12:47 pm


 STAA wa timu ya taifa ya Ufaransa Antoine Griezman amefanikiwa kuibeba timu yake baada ya kufunga bao la kusawazisha dhidi ya Hungary katika sare ya kufungana bao 1-1.

Katika mchezo huo Hungary ndiyo walikuwa wa kwanza kucheka na nyavu dakika ya 45 kupitia kwa nyota wao Attila Fiola na kuwafanya waende mapumziko wakiwa kifua mbele.

N Griezmann ambaye alipachika bao la kuweza usawa dakika ya 66 na kufanya ngoma ikamilike kwa sare ya kufungana bao 1-1.

Ikumbukwe kwamba katika michuano ya Euro 2016 Griezaman alikuwa mfungaji bora baada ya kufunga mabao 6 na Ufaransa ilipoteza kwenye mchezo wa fainali kwa kufungwa na Ureno ambao walisepa na taji hilo.

GONJWA LA AJABU LAMKUMBA KIUNGO WA YANGA KASEKE, FEI TOTO WAWEKA REKODI YAO KWA MKAPA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply