Simba SC

SIMBA YATAJA KILICHOWAFANYA WAKASHINDWA KUPATA MATOKEO MBELE YA YANGA

admin July 4, 2021 2:47 pm


 JOHN Bocco, nahodha wa Simba amesema kuwa sababu iliyowafanya wapoteze mchezo wao wa jana ni kushindwa kutumia nafasi ambazo walizitengeneza.

Ikiwa inanolewa na Kocha Mkuu, Didier Gomes ilishuhudia ubao wa Uwanja wa Mkapa ukisoma Simba 0-1 Yanga katika mchezo wa Kariakoo, Dabi uliokuwa na ushindani mkubwa.

Bocco amesema:”Ilikuwa ni mchezo mkubwa na wenye ushindani ila mwisho wa siku tumeshindwa kupata matokeo mchezo umeisha tunatazama mechi zetu zijazo.

“Haikuwa kazi rahisi nasi tulikuwa tunahitaji pointi tatu hata wapinzani wetu wanahitaji pointi tatu ambazo wamezipata hivyo tutajipanga kwa ajili ya mechi zetu zijazo,” amesema.

Bocco ni mzawa namba moja kwa utupiaji akiwa ametupia mabao 14 sawa na Prince Dube wa Azam FC ambaye ni raia wa Zimbabwe.

NYOTA BERNARD MORRISON AJIRUDISHA YANGA ALIYEWATUNGUA SIMBA AFUNGUKA KUWA WALIKUWA NA JAMBO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply