Kwamba ukiwa Mtanzania kuna mambo fulani ya kawaida tunatazamia uyafanye, lakini kama ukizidisha zaidi ya hapo basi kuna namna ambayo inafanyika nje ya uwanja na sio kwa uwezo wako binafsi.
Kile ambacho alikuwa anakifanya na Bournemouth sasa hivi anakifanya akiwa na Newcastle United. Amepata wachezaji wenye ubora zaidi kuliko wale aliokuwa nao Bournemouth. Na sasa tunaofuatilia soka la Kiingereza tunajua kwamba Newcastle United wanaweza kwenda Top Four.