Habari za michezo

SIKU ZA KISINDA YANGA ZAHESABIKA…KAMBOLE AWEKWA TAYARI KUCHUKUA NAFASI…

admin November 7, 2022 8:15 pm

Yanga tayari ipo Tunisia baada ya kuondoka juzi mchana na kulala Dubai, huku makocha wa timu hiyo wakiwa na presha kubwa ya mechi ya marudiano ya ugenini dhidi ya Club Africain ya huko, lakini Za Ndaani Kabisa zinasema Yacouba Songne na Lazarious Kambole wanarudishwa kikosini.

Kambole na Songne wapo katika kikosi hicho wakilipwa kila kitu, licha ya kutotumika kutokana na kutosajiliwa msimu huu, lakini Za Ndaani Kabisa, zinasema mastaa hao watarejeshwa kikosini rasmi dirisha dogo, wakipishana na baadhi ya nyota waliochemsha kwa sasa watakaotemwa au kutolewa kwa mkiopo.

Nyota wanaoweza kutolewa kwa mkopo ni Joyce Lomalisa, Heritier Makambo, Tuisila Kisinda na Jesus Moloko ambao wamekuwa na viwango vya kawaida tofauti na walivyotarajiwa.

Kutokana na kanuni kwa klabu kuruhusiwa kusajili nyota wa kigeni 12, Yanga inajipanga kuwatoa kwa mkopo au kumalizana kabisa na mastaa hao ili kuwapisha Kambole ambaye alisajiliwa na kukumbwa na majeraha kabla ya kutangazwa kupelekewa Uganda ili kumpisha Kisinda na mwishowe kusalia Jangwani akihudumiwa kila kitu na kama ilivyo kwa Songne aliyekuwa majeruhi wa muda mrefu.

“Kwa namna wachezaji hao wawili wanavyojituma mazoezini, japo hawatumiki, mabosi wameona ni vyema wakaongezwa kwenye dirisha dogo kuchukua wale watakaotemwa au kutolewa kwa mkoko kutokana na kushindwa kuibeba timu kwenye michuano ya ndani na ile ya kimataifa,” kilisema chanzo kutoka ndani ya klabu hiyo.

Inaelezwa kuchemsha kwa baadhi ya nyota waliotumainiwa kuibeba timu Ligi Kuu Bara na michuano ya CAF, imewatibua mabosi wa klabu hiyo na sasa wanapata shinikizo kubwa kutoka kwa mashabiki wanaotaka wapigwe chini kwani hawana msaada.

HIZI HAPA SIKU 60 ZA NDOA YA MGUNDA NA SIMBA…KAWEKA NA KUVUNJA REKODI KIBAO ZA WAZUNGU… KISA KIWANGO CHA OKRAH…SIMBA WAKOSA MAMILIONI KUTOKA FIFA…WANGELAMBA BINGO NONO…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply