Habari za Yanga
Habari za michezo

PAMOJA NA KUWAITA ‘WALA MIHOGO’…INJINIA HERSI APOKELEWA KWA ‘VIBE’ YANGA ..

admin November 12, 2022 12:58 pm

Pamoja na kocha mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi kutafuta njia ya kuwakwepa mashabiki wachache waliopata nafasi ya kuingia ndani ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere jitihada zake zimegonga mwamba baada ya kuonekana na kuimbua shangwe kwa mashabiki wakiimba jina lake.

Nabi ndiye aliyekuwa wa mwisho kushuka kwenye ndege baada ya wachezaji na viongozi wote kutoka na kupanda ndani ya gari la timu tayari kwaajili ya kuelekea Hotelini kula na kujiandaa na safari ya kuwafuata Kagera Sugar.

Mashabiki wamemsindikiza kocha huku wakiwa wanataja jina lake hadi kwenye gari ndogo iliyokuja maalum kwa ajili ya kumpokea.

Yanga inaondoka na Air Tanzania saa moja usiku kwaajili ya kwenda Mwanza kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Kagera Sugar utakaochezwa Jumapili.

HERSI AIBUKA SHUJAA

Mbali na mashabiki kumuimba kocha pia walimtaja rais wa Yanga, Hersi Said kuwa ni kiongozi shujaa ambaye amehakikisha timu inapata matokeo pamoja na maneno mazito aliyotamkia.

Hersi alisema ushindi ni zawadi kwa mashabiki wao ambao walikuwa na maumivu makali kutokana na timu yao kushindwa kupata matokeo kwenye uwanja wa nyumbani.

“Haikuwa rahisi wachezaji walipambana na kufanya kile kilichokuwa kinatakiwa tunawashukuru na kupangeza juhudi zao sasa tumesahau matokeo yaliyopita mipango inaelekezwa kwenye mchezo ujao.” alisema.

NUNUA TIKETI YA USHINDI KWENYE KASINO YA MTANDAONI YA MERIDIANBET… YANGA VS WAARABU…NABI ALIFAULU KWENYE HILI…REFA HAKUWA NA MBAMBAMBA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply