Habari za michezo
FT:KAGERA SUGAR 0-1 YANGA SC….DOGO WA TIMU B AMFUNIKA MAYELE…
admin
November 13, 2022
6:33 pm
KLABU ya Yanga imeendeleza ubabe kwenye ligi kuu Tanzania Bara baada ya kuichapa Kagera Sugar 1-0 kwenye mchezo ambao uliopigwa kwenye dimba la CCM Kirumba Jijini Mwanza.
Yanga Sc imepata bao kupitia kwa nyota wao kinda kabisa Clement Mzize ambaye alipokea krosi nzuri kutoka kwa Feisal Salum katika kipindi cha kwanza cha mchezo na kuisadia timu yake kuibuka na ushindi huo muhimu.
Yanga Sc iliwapumzisha baadhi ya wachezaji wao akiwemo Morrison, Bangala,Aucho na Moloko na kuwapa nafasi baadhi ya wachezaji ambao mara nyingi huwa hawachezi mara kwa mara..
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.