Habari za michezo
UINGEREZA ‘WAUA MENDE KWA RUNGU’…SENEGAL BILA YA MANE YAKUNG’UTWA…
admin
November 22, 2022
7:00 am
Mabao 8 yamepatikana kwenye mchezo wa Kombe la Dunia huko Qatar baada ya dakika 90 kukamilika kati ya England dhidi ya Iran.
Ubao wa Uwanja wa taifa wa Khalifa umesoma England 6-2 Iran kwenye mchezo wa kundi B.
Mabao ya Jude Bellingham dakika ya 35, Bukayo Saka dakika ya 43 na 62, Raheem Sterling dakika ya 45+1, Marcus Rashford dakika ya 71 na msumari wa mwisho ulipigwa na Jack Grealish dakika ya 89.
Msumari wa Grealish ulikamilisha idadi ya mabao 6 huku yale mawili kwa Iran yakifungwa na Mehdi Tarem dakika ya 65 na 90+13 kwa mkwaju wa penalti.
Aidha katika mchezo mwigine, Uholanzi ilifanikiwa kuibuka naushindi dhidi ya Senegal.
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.