Home Habari za michezo HII ‘UNBEATEN’ YA YANGA HAIKUJA HIVI HIVI….KARIBU BILIONI KUMI ZIMETUMIKA…UKWELI HUU HAPA…
- Habari za michezo
- Habari za Yanga
- Habari za Yanga Leo
- Michezo
- Michezo Bongo
- Michezo Soka la Bongo
- news
- Yanga SC
Kocha wa zamani wa Yanga, Mwinyi Zahera wakati timu hiyo inaanza kufumua kikosi aliwahi kusema; “Wakati mwingine lazima ubadilishe gia kwa kutumia hawa wachezaji wenye asili ya Kifaransa. Ni watu wa kazi sana na wana malengo.”
Baadaye waliimarisha zaidi wakiwaingiza Dickson Job, Aboutwalib Mshery, Ibrahim Abdallah ‘Bacca’, Salum Aboubakar ‘Sure Boy. Msimu huu wakawaingiza sita wapya wakiwemo Stephane Aziz KI, Bernard Morrison, Tuisila Kisinda, Lomalisa Mutambala na Gael Bigirimana.
Ukiangalia kuanzia msimu ambao Kocha Nasuruddine Nabi aliipokea timu hiyo kutoka kwa kocha wa muda Juma Mwambusi kuna kiungo mmoja tu amesalia katika timu hiyo mpaka sasa Feisal Salum ‘Fei Toto ambaye ndiye staa aliyekaa ndani ya timu hiyo kwa muda mrefu.
Katika kusimamia usajili wote huo, Yanga dereva alikuwa Hersi Said ambaye akitokea kuwa bosi wa kampuni iliyofadhili maboresho hayo ya GSM mpaka baadaye akawa Rais wa klabu hiyo.
“Posho hizo ziliendelea kuongezeka zaidi mpaka kufika mamilioni, tunafurahia matokeo ya uwekezaji mzuri wa timu kutofungwa, rekodi ambayo sio tu Afrika sasa inapasua mpaka klabu kubwa za Ulaya.”
“Mtaona jinsi ufundi na ubora wa wachezaji unavyozingatiwa, tunashirikiana kwa ukaribu mkubwa wengine nje ni ngumu kuona hili, lakini niseme matokeo yake ni mafanikio kama haya ya ubora yanavyoendelea kujionyesha.
Akizungumzia hatua ya mafanikio hayo ya kikosi chake Nabi alisema hatua ambayo wamefikia ni ndoto zake pamoja na uongozi kujenga kikosi imara na kwamba kwake bado haijafikia katika ubora anaoutaka.