Okwa Akiwa Ihefu
Habari za michezo

OKWA WA IHEFU APANIA KUWAUMBUA SIMBA KWA KUMUACHA DIRISHA DOGO…ISHU YAKE IKO HIVI…

admin March 13, 2023 10:16 am

Kiungo mshambuliaji wa Ihefu, Nelson Okwa amesema kikubwa kwake ni kupata nafasi ya kucheza kwenye mechi zilizosalia ili kuhakikisha anaonyesha kiwango cha kusaidia timu yake.

Okwa anacheza kwa mkopo Ihefu, akitokea Simba iliyomsajili kutoka Rivers United, lakini hakuwa na nafasi kwenye kikosi cha Wanamsimbazi, hivyo akaona aende timu anayoweza kucheza.

Baada ya kutua Ihefu, Okwa amefunga bao moja dhidi ya Dodoma, hivyo anatamani kufunga zaidi kadri atakavyopata nafasi ndani ya kikosi hicho.

“Kikubwa kwangu ni nafasi ya kucheza, ili nifanye kitu kwenye mechi zilizosalia kumaliza msimu huu ambao sikuuanza vizuri,” alisema.

Alikiri Ihefu ina wachezaji wazuri na wazoefu ambao wanaibua ushindani unaompa chachu ya kuendelea kupambana zaidi kwa ajili ya kumalizia msimu akiwa kwenye kiwango kikubwa.

“Ni kiu ya kila mchezaji kufanya vizuri, kwa sababu soka ni kazi yake, hivyo unapokuwepo ushindani inakuwa sababu ya kuongeza umakini na kupambana kuhakikisha uwepo wangu unakuwa msaada kwenye timu,” alisema.

Kocha wa timu hiyo Zuber Katwila alisema “Wachezaji walioingia dirisha dogo wamekuwa na mchango mkubwa ndani ya kikosi hicho ,wanasaidiana na waliopo kuiondoa timu kwenye hatari ya kushuka daraja.”

SIMBA NA YANGA ZAZIDI KUINGARISHA TZ CAF……ISHU IKO HIVI… KUHUSU MZIZA NA NAMNA ANAVYOCHEZA YANGA…NABI KATIKISA KICHWA WEE..KISHA AKASEMA HAYA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6131

Leave a Reply