Habari za Simba SC
Habari za michezo

SIMBA WAZIDI KUIFUNIKA YANGA KWA PESA BONGO…DILI JIPYA LA MIL 500 HILI HAPA…

admin March 23, 2023 8:08 pm

Kampuni ya MobiAd Afrika leo imetangaza kudhamini Timu ya Vijana ya Simba kwa mkataba wenye thamani ya Tsh. Milioni 500 kwa miaka miwili ambao unalenga kukuza Soka la Vijana.

CEO wa MobiAd Africa, Rumisho Shikonyi amenukuliwa akisema “Tumeona hii ni fursa kuungana kwenye hii safari, tunatangaza udhamini kwa Timu ya Vijana ya Simba Sports Club kwa mkataba wenye thamani ya Tsh. Milioni 500 kwa miaka miwili, tunaamini mpira wa miguu ni sehemu ya suluhisho la ajira kwa Vijana, Simba ni Timu kubwa Afrika na inazidi kuwa kubwa hivyo ni vizuri kuandaa Vijana ambao watachukua nafasi ya hawa wa sasa”

CEO wa Simba, Imani Kajula amesema “Soka la Vijana ni muhimu sana ili uwe na Timu ya Vijana iliyo bora lazima iwezeshwe, kama ilivyo kwa Wachezaji wengine kama Mohamed Hussein kutoka kwa Timu ya Vijana”

“Simba inakwenda mbele kutambua vipaji, kuvichukua na kuviendeleza na kuweza kutengeneza Timu yenye vipaji vikubwa sana, tunaamini Simba imara yenye vipaji haitaisaidia Simba pekee bali hata Taifa letu”

Kwa upande wake , Ahmed Ally amesema ““Tunakwenda kubadili taswira ya mpira wa Vijana, uzuri tunajua tunachofanya,  ndio tumetoa Vinana wengi ambao wanafanya vizuri kwenye Timu za Ligi Kuu na Ligi Daraja la Kwanza, tunao Watu ambao wanajua namna ya kukuza Soka la Vijana

SIKU CHACHE BAADA YA SIMBA KUIZABUA HOROYA 7-0…TRY AGAIN AFUNGUKA MAGUMU WALIYOPITIA… PAMOJA NA MAZEMBE KUPOTEANA CAF…NABI KAITAZAMA WEE..KISHA AKASEMA HILI KWA MASTAA WA YANGA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply