Tetesi za Usajili Yanga
Habari za michezo

KUHUSU MAMELOD SUNDOWNS KUMTAKA MAYELE…UKWELI WOTE HUU HAPA…YANGA HAWAWEZI KUCHOMOA HAPA…

admin May 23, 2023 4:56 pm

Inasemekana mabingwa wa ligi kuu nchini Afrika Kusini (PSL) Mamelodi Sundowns wameanza harakati za kuhakikisha wanainasa saini ya mshambuliaji nyota raia wa Congo DR na klabu ya Young Africans, Fiston Kalala Mayele.

FARPost inaweza kuthibitisha kwamba ripoti ya kina ya skauti iliwasilishwa kuelekea mwisho wa 2022. Hata hivyo, bado hakuna makubaliano ndani ya klabu kwa wakati ule kwamba Mayele atafaa style yao ya uchezaji hiyo, ilionekana ni vigumu kwa Sundowns kumtafuta nyota huyo wa Yanga.

Lakini mwaka huu Rulani Mokwena anaonekana kuvutiwa sana na anamhitaji Mayele kwa udi na uvumba ili akasaidiane na Peter Shalulile.

Inasemekana juzi akiwa Rustenburg wiki iliyopita kabla ya mechi ya marudiano ya nusu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Marumo, aliripotiwa kutembelewa na mwakilishi wa Sundowns.

Tayari matajiri hao wa Kusini mwa Afrika almaarufu kama “Masandawana” wameshatenga fungu la kutosha kwa ajili ya mshambuliaji huyo kinara wa mabao kwenye ligi kuu nchini Tanzania pamoja na kombe la shirikisho Afrika.

Kwa ubora ambao Fiston Mayele ameuonyesha tangu atue nchini ni lazima aingie kwenye matamanio ya vigogo wengi sana wa soka hapa barani Afrika.

KISA YANGA KUTINGA FAINAL YA CAF…MANARA ATAKA MASTAA WOTE WAFUNGIWE NDANI…AKUMBUSHA YA SIMBA… BAADA YA KUWATAZAMA YANGA…KOCHA WA USM ALGER KANUGA WEE..KISHA AKASEMA HAYA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply