Azam FC
Azam FC

MASTAA AZAM KULAMBA MIL 100 WAKIMBATUA YANGA LEO…

admin June 12, 2023 3:01 pm

Wachezaji wa Azam FC wametengewa Shingili Milion 100 na Uongozi wa Klabu hiyo endapo watafanikisha kutwaa Ubingwa wa Kombe la Shirikisho la Tanzania Bara ‘ASFC’ dhidi ya mabingwa watetezi Young Africans kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga baadae leo Jumatatu (Juni 12).

Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya Azam FC kimeeleza kuwa wachezaji watapewa fedha hizo huku wakiahidiwa tofauti na za benchi la ufundi hivyo kazi imebaki kwao kutimiza lengo.

“Viongozi wameweka kiasi hicho ingawa wameahidiwa kuna uwezekano zikaongezeka, hivyo hizo ni za awali tu, ASFC ndilo taji pekee lililobaki kwetu na hatutaki kulipoteza,” kimeeleza chanzo hicho.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam, Abdulkarim Amin ‘Popat’ amesema hakuna asiyejua umuhimu wa mchezo huo na wao viongozi tayari wameshatimiza wajibu kwa wachezaji wa timu hiyo.

“Kila mchezaji anajua ahadi ambayo sisi kama viongozi tumeiweka lakini siwezi kusema ni kiasi gani, jukumu limebaki kwao kuhakikisha taji hili wanalipigania ili kumaliza msimu kwa heshima.”

Azam FC ilitinga fainali hiyo baada ya kuifunga Simba mabao 2-1 wakati Young Africans ikiitoa Singida Big Stars kwa bao 1-0 la mtokea benchi, Fiston Kalala Mayele.

WAKATI WATU WAKIMUONA ONYANGO MZEE…HAWA HAPA MASTAA WAZEE ZAIDI YAKE LIGI KUU NZIMA… BAADA YA OKRAH….MASTAA WENGINE WANAOTEMWA SIMBA KUJULIKANA LEO….MBRAZILI ASEPA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply