Kocha Msaidizi Simba SC
Habari za michezo

ISHU YA SIMBA NA MGUNGA BADO PASUA KICHWA…MWENYEWE AWAWEKEA NGUMU MABOSI…

admin July 18, 2023 4:50 pm

HUKO Simba hali sio shwari kwa aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Juma Mgunda baada ya kuonekana akiwa na kikosi cha vijana.

Mgunda ameshuhudiwa akiwa kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo Mbweni wakati wa kutafuta vipaji vitakavyojiunga na timu hiyo chini ya kocha mkuu, Selemani Matola na mkuu wa programu za soka la vijana, Patrick Rweyemamu.

Mgunda ambaye hakusafiri na Simba kwenda nchini Uturuki kwa ajili ya maandalizi ya msimu, amekuwa kwenye sintofahamu kubwa kuhusiana na hatima yake ndani ya timu hiyo inayonolewa na Mbarazili, Roberto Oliveira ‘Robertinho’.

Taarifa za mwanzo zipo  zinaeleza Mgunda alitakiwa kupewa timu ya Simba Queens jambo ambalo hata hivyo yeye mwenyewe ilielezwa hayuko tayari kufundisha kwa upande huo kwenye soka la wanawake.

Kuonekana kwa Mgunda kwenye soka la vijana kunaibua maswali mengine ingawa hata hivyo viongozi wa Simba bado hawajaweka wazi cheo chake kipya.

Mgunda alijiunga na Simba Septemba 7, mwaka jana akitokea Coastal Union baada ya timu hiyo kuachana na Zoran Maki aliyesitishwa mkataba wake.

KUHUSU ISHU YA MIQUISSONE NA SIMBA…’UPDATE’ MPYA HIZI HAPA KUTOKA AL AHLY YA MISRI… ISHU YA MBRAZILI KUSEPA KAMBI YA SIMBA UTURUKI…UKWELI USIOSEMWA HUU HAPA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply