Habari za Yanga
Habari za michezo

YANGA YA MSIMU HUU NI HATARI CHEKI ILICHOFANYA KWENYE MECHI ZA KUJIPIMA LEO

Staff Desk August 4, 2023 2:07 pm

Yanga imeendelea na maandalizi yake kuelekea msimu ujao ambapo leo itakuwa na mechi mbili za kirafiki za kujipima nguvu.

Asubuhi ya leo Yanga imecheza na timu ya Friends Rangers ya jijini Dar es Salaam na mabingwa hao wa Ligi Kuu msimu uliopita wakishinda kwa mabao 6-1.

Mabao ya Yanga yamefungwa na washambuliaji Crispin Ngushi aliyefunga mara mbili, Clement Mzize na Hafiz Konkoni, Pacome Zouzoua na Stephanie Aziz KI.

Konkoni huo ni mchezo wake wa kwanza wa kirafiki tangu asajiliwe na Yanga wiki iliyopita akianza vyema kwa kufunga bao hilo.

Leo tena jioni Yanga itacheza mchezo mwingine wa pili wa kirafiki watakapokutana na JKU ya Zanzibar.

Kabla ya mechi hiyo ya JKU Yanga imeshacheza mechi nne za kirafiki wakishinda zote ambapo mchezo wa kwanza ulikuwa dhidi ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini (1-0), Magereza Dar (10-0), Friends (6-1) na kufanya timu hiyo kufunga jumla ya mabao 17 huku wao wakiruhusu bao 1.

Yanga imeweka Kambi yake ya maandalizi kambini kwao AVIC TOWN Kigamboni huu ukiwa msimu wa pili sasa wakijiandaa eneo hilo hilo.

GAMONDI AFUNGA PRE-SEASON YANGA KIBABE….. JUMATATU TANGA HAPAKALIKI ROBERTINHO AFUNGUKA SABABU HIZI 10 KWA SIMBA KUWA BINGWA MSIMU HUU

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply