Habari za Simba
Habari za michezo

KISA SARE NA POWER DYNAMO JANA….MBRAZILI SIMBA APATA CHA KUJITETEA….

admin September 17, 2023 10:22 am

Kocha Mkuu wa Simba , Roberto Oliviera ‘Robertinho’ amesema wamepoteza nafasi tano za wazi za kufunga katika sare ya 2-2 dhidi ya Power Dynamos ambazo zingetuwezesha kupata ushindi mnono ugenini.

Robertinho amesema kipindi cha pili timu yake ilicheza vizuri na kutengeneza nafasi nyingi ambazo hwakuzitumia vizuri.

Hata hivyo Robertinho amewapongeza wachezaji kwa kazi kubwa waliyofanya katika mchezo wa jana licha ya kupata sare.

“Tumecheza vizuri hasa kipindi cha pili, tumetengeneza nafasi nyingi. Tumepoteza nafasi zaidi ya tano za kufunga lakini huu ndio mpira wa miguu tunarudi nyumbani kujipanga,” amesema Robertinho.

Kwa upande wake, mlinzi wa kati Che Fondoh Malone amesema bado wanafasi ya kufanya vizuri katika mchezo wa marudiano jijini Dar es Salaam hivyo wanarudi kujipanga.

“Hatujakata tamaa ya kusonga hatua ya makundi, tuna dakika 90 nyingine nyumbani ambazo tunaamini tutazitumia vizuri na kuingia hatua ya makundi,” amesema Che Malone.

KIWANGOO! YANGA WAANDIKA REKODI….MUSONDA,MZIZE WAIUA AL MAREIKH CHAMA AWEKA REKODI YA KIBABE NYUMBANI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply