Habari za michezo

KUISHUHUDIA SIMBA VS ASEC NI BUKU 5 TU

Staff Desk November 16, 2023 4:59 pm

Klabu ya Simba imetangaza viingilio vya mchezo wao wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Asec Mimosas utakaochezwa siku ya Novemba 25, 2023 katika dimba la Benjamin Mkapa.

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Klanbu ya Simba, Ahmed Ally, amebainisha kuwa viingilio kwa mzunguko ni Tsh 5000, VIP C Tsh 10,000, VIP B Tsh 20,000, VIP A Tsh 30,000 huku viingilio kwa Platinum vikiwa Tsh 150,000.

Miamba hiyo ya Ivory Coast inatarajiwa kutua Nchini Novemba 23, 2023 wakiwa na msafara wa watu 31. Waamuzi wa mchezo huo utakaopigwa majira ya saa 10:00 jioni watatoka Nchini Misri.

PAMOJA NA MATARAJIO MAKUBWA…CHILUNDA APEWA ‘MAKAVU LIVE’ SIMBA…. SIMBA WASHAURIWA WAACHANE NA SAIDO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply